... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Msingi wa Toba

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favourites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

Matendo 2:38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Listen to the radio broadcast of

Msingi wa Toba


Download audio file

Swali, Kama Mungu anasamehe dhambi zetu kupitia sadaka ya Yesu alipomwaga damu yake pale msalabani, sasa ni kwanini ni lazima tubadilishe mienendo yetu na kuacha dhambi zilizokuwa zimetutenganisha na Mungu mwanzoni … kwani…sadaka yake bado inatosha?

Hili ni swali wale wanaomwamini Yesu huwa wanalikwepa.  Kwa vyo vyote vile, kama msamaha wa Mungu uko kwenye msingi wa kazi Yesu aliyotutendea; na si kwa matendo yetu mema (na mimi ninaamini havyo), kumbe tunaweza kuendelea kuishi kama zamani!.  Lakini.. hilo linaweza kuwa ni jibu sahihi?

Swali lingine ni hili, je!, mwanaume aliyeoa hatakiwi kukutana kimwili na wanawake wengine?…Jibu ni NDIO, mbali na kuwa na cheti cha ndoa, kimantiki, mwanamke aliyeolewa anatazamia mume wake awe mwaminifu kwake siku zote.

Na ndivyo ilivyo kwa Mungu.  Uthibitisho wa imani hauko kwenye sala ya toba tu anenayo mtu kwa midomo yake, bali ni kwa kupitia mwenendo wake uliobadilika.

Matendo 2:38  Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Je!, Ni jambo gani ambalo Petro aliwaambia  watu (wale wale waliopiga kelele wiki chache kabla, “Asulubiwe!”)?

Alisema, Tubuni!  Yaani, Achana na dhambi zenu.  Ni ushahidi kwamba unamwamini Yesu, si kwenye akili tu, lakini na moyo wako wote.  Ni uthibitisho kwamba wewe ni mwaminifu kwake.

Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu.  

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.