Sikiliza Kwanza, Halafu Ndipo Uongee
We're glad you like it!
Enjoying the content? You can save this to your favourites by logging in to your account.
Mithali 18:2 Mpumbavu hapendezwi na ufahamu; ila moyo wake udhihirike tu.
Je! Umewahi kujiona uko sahihi kabisa—kiasi kwamba unajiamini mno, unajigamba hadharani, na kutangaza maoni yako kana kwamba huo ndio “ukweli” usiopingika—bila kusubiri kwanza au kuwasikiliza wengine?
Naam, bila shaka umewahi kuropoka hivyo. Hata mimi pia.
Na ukweli ni kwamba, haipendezi hata kidogo.
Zamani, mwaka 1520, Mfalme Christian wa Pili wa Denmark aliwalika waheshimiwa wa Sweden kuhudhuria “karamu ya amani” mjini Stockholm, baada ya kujidai kwamba amewashinda kwenye vita.
Washauri wake walimwonya kuwa mpole na mwenye busara, lakini hakuwasikiliza.
Badala yake, alitoa hotuba kali sana, akiwashutumu waheshimiwa hao kuwa waasi.
Ndipo akaamuru watu 80 kati yao wauawe — tukio lililokuja kujulikana kama “Maangamizi ya Stockholm.”
Alidhani kufanya hivyo kungethibitisha mamlaka yake, lakini mambo yakamgeukia vibaya.
Watu wa Sweden waliinuka, wakafanya mapinduzi, wakajikomboa, na Denmark ikapoteza utawala wake.
Hatimaye, Christian mwenyewe aling’olewa madarakani.
Laiti angewasikiliza kwanza, pengine angeendelea kutawala nchi zote mbili.
Mithali 18:2
Mpumbavu hapendezwi na ufahamu; ila moyo wake udhihirike tu.
Naona tumepata mfano halisi, sivyo?
Mfalme wa Denmark alijionyesha kuwa mpumbavu katika mazingira yaliyohitaji hekima.
Na hata sisi, ni mara ngapi tumejionyesha vivyo hivyo — kwa kuropoka maoni yetu bila kusikiliza kwanza?
Tunadhani tunajua kila kitu, tunataka kuwafundisha wengine, lakini mara nyingi tunashindwa kutambua hali halisi na kuangukia kwenye makosa makubwa.
Kama tunasubiri tu ili tuseme, bila kusikiliza, tunapoteza hekima.
Usikivu ndiyo njia ya wenye busara; kuropoka ni njia ya wapumbavu.
Hii ndiyo ramani Mungu aliyoitupa kuhusu mawasiliano:
Sikiliza kwanza.
Ni kinyume na silika ya mwanadamu, lakini ndicho kitu kinachojenga amani na maelewano ya kweli.
Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.
