... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Unabii – Je! Ni Kweli au Si Kweli?

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favorites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

Warumi 1:5 Ambaye katika yeye tulipokea neema na utume ili mataifa yote wapate kujitiisha kwa imani, kwa ajili ya jina lake.

Listen to the radio broadcast of

Unabii – Je! Ni Kweli au Si Kweli?


Download audio file

Kuna watu wengi ninawasoma kwenye mtandao wakijidai wao kuwa ni mitume, manabii na kadhalika.  Ndio, ni kweli hivyo ni vipawa Agano Jipya linavyotaja.  Lakini vyote ni halali?  Je!  Vyote ni vya kweli?

Si jambo jipya kwamba ukweli wa Injili ya Kristo unapotoshwa na kubadilishwa na watu wanaotafuta fedha ya aibu.  Huwa imetokea tangu makarne mengi. 

Lakini katikati ya hawa wasiofaa, bado kuna walioitwa na Mungu kweli kweli ili wazitangazie jamii mapenzi ya Mungu, kama nilivyosema, Agano Jipya linaweka bayana kwamba kuna mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji na walimu (Waefeso 4:11). 

Sasa mtu anawezaje kujijua yeye ni nani hasa?  Ni wapi wanatangaza ukweli wa Mungu pamoja na mapenzi yake, na ni wapi wanaupotosha ukweli kwa faida zao wenyewe? 

Basi tunapata jibu kwenye mstari Mtume Paulo alioliandikia kanisa la Rumi zamani kwenye karne ya kwanza baada ya Kristo. 

Warumi 1:5  Ambaye katika yeye tulipokea neema na utume ili mataifa yote wapate kujitiisha kwa imani, kwa ajili ya jina lake. 

Paulo alidai kuwa mtume na kazi za mtume si zingine, ni kuongoza watu mahali pote kumwamini na kumtii Yesu, na kufanya yote kwa kumheshimu Kristo. Nimesikia imesemwa kwamba ni kama tumetengeneza utamaduni wa unabii unaotawaliwa na kumsikiliza Mungu kwa kumtii. 

Na kwa sehemu kubwa hii ni kweli.  Kama mtu anadai kuwa anamsemea Mungu, ni lazima  aweke imani yake ndani ya Yesu na kutii Neno lake.  La sivyo, usimsikilize. 

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.